Dec 20, 2010

serengeti boys yachapwa 1-0


Timu ya vijana ya Tanzania Serengeti Boys imepoteza mchezo wake wa kwanza dhidi ya Rwanda katika mashindano madogo ya Cecafa U-17 yanayofanyika kwenye uwanja wa Amahoro.

Kocha wa Tanzania Jamhuri Kiwhelu amesema kuwa Timu yake ilicheza vizuri licha ya kufungwa bao hilo la penati.

Dec 17, 2010

Kobe na kumbukumbu za alikotoka..


kobe amemshukuru kocha wake wa High school Gregg Downer kwa kumfundisha mambo mengi ambayo yamemfanya awe na mafanikio aliyonayo leo

Kocha  Downer bado anafundisha timu ya shule ile ile ambayo alisoma Kobe inayojulikana kwa jina la Merion High School iliyopo Philadelphia.

Kwa kuonyesha shukurani zake kwa kocha wake huyo Kobe anatarajia kutembelea shule hiyo Alhamisi ijayo kuhudhuria sherehe kwenye gym ambayo wameipa jina lake. Kobe ameahidi kiasi cha $411,000 kwa ajili ya maendeleo ya elimu na michezo katika shule hiyo.

Dec 16, 2010

Mhhhhhhhhh...


hii ilitokea huko Bogota mwaka 1997 huyu bwana Manalo Beltran sijui alitoka hapo akiwa na hali gani maana hilo gombe lilimpania kweli...!!

Forlan apewa Adidas Golden Ball


Mshambuliaji Diego Forlan wa Uruguay amekabidhiwa rasmi tuzo ya mchezaji bora wa Kombe la Dunia inayoitwa Adidas Golden Ball baada ya kuchaguliwa kuwa mchezaji bora katika Fainali za Kombe la Dunia zilizomalizika nchini Afrika Kusini.

Forlan alikabidhiwa tuzo hiyo na mchezaji mkongwe wa soka Franz Beckenbauer katika sherehe iliyofanyika nchini Ujerumani.

Dec 15, 2010

..KISASI AU?




ouchhhh...
hawa jamaa wana bifu au hii ni ajali tu?

Dec 14, 2010

MTANGAZAJI AULA TFF..


Mtangazaji wa Kituo cha EATV, Jimmy Kabwe ameibuka kidedea katika mchakato wa kusaka Mkurugenzi wa Masoko wa TFF, Rais wa TFF Leodegar  Tenga amewaambia Waandishi wa Habari  kuwa Jimmy Kabwe ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Masoko wa TFF.

Dec 8, 2010

HII KALI....


Ingekuwa poa kweli kama magorofa kama haya yangejengwa karibu na Neshno stadium, tungekuwa hatuna tabu ya kulipa miviingilio....
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...