Nov 29, 2012

MADHARA YA UTUMIAJI WA MIRUNGI (khat)

 
Matatizo na madhara ya Mirungi yaligunduliwa mwanzo katika mwaka 1935 na League Of Nations, Mwaka 1970 taasisi ya tiba ikaitenga madhara ya cathinone yanayopatikana katika Mirungi ambayo kikemikali inafanana na amphetamine, na hivyo katika mwaka 1971 ikaorodheshwa na United Nation kuwa ni miongoni mwa madawa ya kulevya.
 
mirungi

 
Utumiaji wa Mirungi husababisha madhara mbalimbali kiafya kama:
  1. Magonjwa ya vidonda vya tumbo (ulcers)
  2. Ukosefu wa haja kubwa (constipation)
  3. Utumiaji wa muda mrefu husababisha kuharibu utendaji kazi wa ini, na pia kusababisha ubadilikaji rangi meno, kudhoofika, na fizi kuuma na harufu ya mdomo
  4. Upungufu wa msukumo wa kufanya jimaa (sex drive). Na pia kuwahi kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu;
  5. Kupatwa na ugonjwa wa futuru/futuri/bawasiri/baasili – nyama inaoota kwenye utupu wa nyuma
  6. Upungufu wa usingizi
  7. Humpelekea mlaji kutawaliwa nayo (Addiction)
  8. Walaji wengi huvuta na sigara, hata yule aliyekuwa havuti kabla ya kuanza kula Mirungi, hujikuta akizama kwenye uvutaji, na madhara huwa maradufu

 
mirungi
 
mirungi hujulikana pia kwa majina mbalimbali kama vile gomba, shamba, miraa, khat na kadhalika

Nov 27, 2012

sharo milionea afariki dunia...

Habari zilizoifikia blog ya cheyfitness hivi punde zinaripoti kwamba Msanii-Muigizaji wa filamu na mchekeshaji nchini maarufu kwa jina la "Sharo Milionea" amefariki dunia kwa ajali mbaya ya gari iliyotokea huko Lusanga, Muheza mkoani Tanga majira ya saa  2 usiku jana,

     Hussein Mkiety aka sharo milionea
 
Uongozi wa Blog ya cheyfitness unatoa pole kwa ndugu,jamaa, marafiki na watanzania wote kwa ujumla

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi....Amen.

Nov 26, 2012

FAIDA ZA SABUNI YA LIWA (sandalwood soap)

historia ya matumizi ya mti wa liwa katika kuboresha na kuipa afya ngozi inaanzia zamani sana katika nchi za Egypt, China na India...kwa miaka mingi sana inajulikana kwa uwezo wake wa kuboresha ngozi na kuipa afya...liwa imeweza kutengenezwa katika mionekano mbalimbali kama mafuta, maji ya liwa na sabuni....
 
kwa wale ambao hawajawahi kuuona mti wa liwa ndio huu unakua mkubwa kabisaaaa
 

tukizungumzia sabuni ya liwa ambayo ina faida nyingi katika ngozi zetu ambazo ni:
i)  kulainisha ngozi
ii) kufanya ngozi iwe nyororo na yenye afya
iii)pia inasaidia kuondoa muwasho, harara, vipele na harufu mbaya

sabuni ya liwa


jamani hizi sabuni ni nzuri sana na zina saidia sana kama una vijimatatizo vya hapa na pale vya ngozi na unataka kuboresha ngozi yako basi jaribu kuogea sabuni ya liwa

NB: kama ukitumia liwa na ukiona inakuharibu ngozi badala ya kuipa afya acha kuitumia mara moja na umuone daktari

Nov 14, 2012

VITUKO MICHEZONI

 
 
huyu sijui atatua vipi jamani maana matairi ndio hayoooooo


 
huu ni mchezo gani jamani.....mmmh


Nov 13, 2012

nimerudi tena

habari zenu wapenzi wa blog hii,

nawaomba radhi kwa kupotea na kutokuandika kwa muda mrefu ni mambo yaliyokuwa nje ya uwezo wangu yaliyosababisha hali hiyo
lakini sasa nimerudi tena na nguvu mpya...
pamoja sana

karibuni tena
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...