Jan 25, 2010

MAZOEZI YA VIUNGO


mazoezi ya viungo ni shughuli inayotakiwa kufanyika mara kwa mara ili kuboresha na kutunza ubora wa miili yetu. mazoezi ya viungo yanakuwezesha kufanya shughuli za kila siku kwa ufasaha na bila kupata uchovu uliopitiliza, pia mazoezi ya viungo yanasaidia kutufanya tukabiliane vyema na 'stress' za kila siku pamoja na kutupa wepesi katika matukio yanayohitaji uharaka wa kutenda.


ufanyaji wa mazoezi ya viungo mara kwa mara yanasaidia kutuepusha na maradhi ya mara kwa mara na kuwa na afya bora. Mazoezi yapo ya aina mbalimbali na kuna jinsi tofauti za kufanya mazoezi hayo kwa hiyo kila mtu anaweza kushiriki kwenye mazoezi kwa njia moja ama nyingine.

2 comments:

  1. mimi nataka nifanye mazoezi ya kupunguza tumbo maana nina tumbo kubwa sasa ningeomba unionyeshe mazoezi ya kupunguza tumbo mpz.. tunashukuru kwa kutuwekea mambo mazuri kwenye blog yako...kazi njema na siku njema.

    ReplyDelete
  2. mimi pia natak kujua jinsi ya kupunguza tumbo.asante

    ReplyDelete

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...