Jan 26, 2010

TFF : Tiketi za kombe la Dunia zimeisha


Shirikisho la Soka Nchini (TFF) jana limesema tiketi zote 30 ambazo Tanzania imepewa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) kwa ajili ya mashabiki wa Tanzania kuona mechi ya Fainali za Kombe la Dunia itayofanyika Julai 11 nchini Afrika Kusini zimeshauzwa ambapo tiketi ya daraja la kwanza imeuzwa Dola 900ambazo ni sawa na Sh. Milioni 1.2

Afisa Habari wa TFF amesema kuwa tiketi kwa ajili ya hatua nyingine za mashindano hayo bado zipo nyingi za kutosha kwani kuna tiketi 60 kwa ajili ya mechi Na. 2 hadi Na. 48. Tiketi 30 za mechi ya ufunguzi ambayo itakuwa baina ya wenyeji Afrika Kusini na Mexico kwenye Uwanja wa Soccer City mjini Johanesburg pia zimeshauzwa zote.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...