Feb 2, 2010

Simba SC yaichapa Toto


Simba jana iliendelea kudhihirisha ubabe wake katika ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa Toto Africa ya hapa mabao 2-0 katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mjini Mwanza.

Mussa Hassan 'Mgosi' ndiye aliyepachika bao la kwanza katika dakika ya 52 na dakika mbili baadaye Ramadhani Chombo 'Redondo' aliimaliza Toto baada ya kupachika bao la pili.

katika mechi ya jana kulikuwa na imani za kishirikina ambapo Simba walidai kukuta chumba choa kimemwagiwa vitu vya majimaji vyekundu vinavyofanana na damu, hali iliyomlazimu Katibu Mkuu wa Simba Kaduguda kumuandikia barua Kamisaa wa mchezo huo kwamba hawatatumia chumba chao kutokana na tukio hilo.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...