Feb 3, 2010

Unamkumbuka? SULEIMAN NYAMBUI

Suleimani Nyambui alizaliwa Februari 13, 1953, ni mkimbiaji mstaafu kutoka hapa Tanzania ambayealishinda:
  • Medali ya Shaba katika All-Africa Games mwaka 1978.
  • Medali ya Fedha katika mbio za mita 5,000katika Summer Olympics mwaka 1980.
  • Alishinda mara mbili Berlin Marathon mwaka 1987 na 1988.

Alihudhuria University of Texas at El Paso (UTEP) mwaka 1978-1982 ambapo alishinda mara nne 'titles' za NCAA (National Collegiate Athletic Association) kwenye mbio za mita 10,000 na mara tatu kwenye mita 5,000.

katika michezo ya Millrose iliyofanyika New York, Februari 1981 Nyambui alivunja rekodi ya dunia ya mbio za mita 5,000 kwa kukimbia kwa dakika 13:20.4

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...